Tuesday, 7 May 2013



JE!UNAJUA MZUNGUKO WA MAISHA YA NYUKI?

Mzunguko wa maisha ya nyuki upo katika ngazi 4 yaani..(a)yai{egg} (b)kiluwiluwi{larva} (c)buu{pupa} (d)nyuki kamili{adult}.ukuaji huu unaanza na yai ambalo malikia anatunga na mara tu anapotoka kujamiiana na nyuki dume{drone}. Naukuwaji huu wa nyuki kutoka yai hadi kuwa nyuki kamili huwa una tofautiana na jinsia gani ya nyuki itakayo zalishwa.

kwani kuna aina 3 za makundi {caste} za nyuki 1.worker{kibarua} 2.malikia{queen} 3.nyuki dume{drone}.

zifuatazo ni hatua mabazo caste hawa hupitia kutoka yai hadi kuwa nyuki kamili.

1.worker{kibarua}

HATUA

(a)YAI{EGG}

-hapa yai linaanguliwa kwa muda (siku) 3.

(B)KILUWILUWI{LARVA}.

Katika hatua hii lava mabadiliko ya ngozi yana tokea mara 4 ila kwa muda (siku) tofauti.mageuzi ya kwanza ya ngozi muda (siku)3.5 , mara ya pili muda (siku) 4.5 ,mara ya tatu muda ( siku)6.5 ,mara ya nne ambayo ni badiliko la mwisho kwa hatua hii ya lava ambao huchukua muda (siku)6.5. baada yahapo chumba cha sega cha lava kinafunikwa na nta kwenye muda (siku)8-9.

(C)BUU{PUPA}

-Hapa mambo mawili hutendeka  kwa muda(siku) tofauti.

*pupa hujizungushia mfuko wa nyuzi nyuzi muda (siku) 10.

*pupa kujigeuza ngozi kwa mara ya 5 muda (siku)11. 

(D)NYUKI KAMILI{ADULT}

-Hapa mabadiliko ya ngozi yanafanyika kwa mara ya mwisho na kuwa nyuki kamili  na mabadiliko hayo yanafanyika kwa muda (siku)20.

-Na wa muda(siku)21 anatoka nje ya chumba ambacho alikuwa analelewa na kuwa nyuki kamili.  

2. MALIKIA{QUEEN}.

HATUA

(a)  YAI{EGG}

- Muda (siku) 3 yai linaanguliwa.

(b) KILUWILUWI(LARVA)

 -Hap mabadiliko ya ngozi yanatokea kwa muda (siku) tofauti kwani mbadiliko wa 1 hufanyika muda ( siku) 3.5 ,wa pili ni 3.5 , wa tatu ni 6.5 ,wa nne ni 6.5 , na baada ya hapo muda (siku) 8 chumba cha malikia{queen cell} kinafunikwa na nta .

(C)BUU{PUPA}

-Muda(siku) 10 anajizungushia mfuko wa nyuzi

-Na muda(siku) 10 anafanya tendo la kujigeuza ngozi kwa mara ya  5.

(D)NYUKI KAMILI{ADULT}.

-Muda (siku) 15 anajigeuza ngozi kutoka buu kuwa nyuki kamili   -Muda (siku) 16 anatoka kwenye chumba chake {queen cell} teari kwa kujamiana na nyuki dume{drone}.

3.NYUKI DUME{DROME}.

HATUA.

(A) YAI{EGG}.

-Muda (siku) 3 yai linaanguliwa .

(B)KILUWILUWI{LARVA}

-Hapa lava anajigeuza ngozi mara 4 ila muda (siku) tofauti

*Kwa mara ya  kwanza  muda (siku)4

*Kwa mara ya pili muda(siku)5

*Kwa mara ya tatu  muda(siku)7

*Kwa mara ya nne  muda(siku)7

-Muda(siku)10 chumba cha nyuki dume kina funikwa na nta .

(C)BUU{PUPA}.

-Muda(siku)12 buu anajizungushia mfuko wa nyuzi nyuzi.

-Muda(siku)14 tendo lakujigeuza ngozi kwa mara ya 5 lina tendeka.

(D)NYUKI KAMILI{ADULT}.

-Hapa buu anajigeuza ngozi na kubadilika kuwa nyuki kamili  muda(siku)225.

-Muda(siku) 24 nyuki dume (drone) anatoka nje ya chumba {drone cell} teari kujamiana na malikia{queen} .

No comments:

Post a Comment